Ndoa Nyingi Zinavunjika Kutokana Na Mambo Yanayoweza Kuzuilika


Unapouliza Sababu kubwa ambayo inasababisha ndoa kuvunjika , watu wengi utasikia wakisema, Ni kwa sababu ya Utofauti wao, wamekua mahali tofauti.Hakuna kitu ambacho ni cha kawaida. Ingawa  wengi hawaelewi  kwamba  kuna sababu za kuzuilika.

Kutokana na uchunguzi uliofanyika ,ndoa nyingi zinavunjika kwa sababu ya kuwa na uchumi mbaya. Karibu asilimia 20 wanasema hivyo kuwa Pesa ndio chanzo.Lakini kwa nini? Ikiwa watu wengi watafahamu kipato cha mwenza kabla ya kujiingiza kwenye Kiapo. Kuweka sawa matarajio yao, kukubaliana katika mahitaji yao. Inakuwaje tena  hawa watu washindwe kuelewana kwa sababu ya pesa? Inakuwaje washindwe kutimiziana?

Fikiria hivi vitu ambavyo vinawaweka hawa watu pamoja: Wanashirikiana interest zao, vipaumbele vyao, mtindo wa maisha  walionao. Kitu watu wanachosahau ni  au kutambua ni kwamba jinsi unavyoitumia pesa yako ndivyo ilivyo sehemu kubwa ya maisha yako. Lakini, Pia ni jinsi gani unavyotumia weekend yako, Tabia ya uchumi  sio kitu ambacho  utagundua kwa urahisi unapokuwepo kwenye mahusiano ya mwanzo.

Hio ni kweli kwa sababu kama mwenza wako yuko vizuri katika  kuficha idadi ya pesa alizonazo utajuaje kiasi alichonacho?

Kufahamu hilo jambo la pesa , inaondoa tofauti zote, bila ya kufikiria kitu kingine, kuliko wale ambao wanaficha  hata kabla hamjaoana, hujui mwenza wako ana kipato gani, huo ni ujinga mkubwa . Ndio maana pesa inasababisha kuvunjika kwa ndoa.

Wanandoa Wenye Mafanikio ,Walijua Haya Yafuatayo kabla ya Kuoana.

Wanafahamu kiwango cha kipato cha mwenza

Wanafahamu malengo ya wenza wao

Wanafahamu  matarajio  na hamu ya wenza wao

Wanakuwa tayari wamejaa taarifa kamili kuhusu ndoa

Wanakuwa wamekamilika kila mahali, wanajipenda,  wanajijali, wamejikubali

Hio ndio njia ya kuwapenda na kuwajali wengine.

Ni waelewa. kila mtu anamuelewa mwenzake.

Unaweza kushangaa kama nikikuambia kuwa mawasiliano ndio Msingi mkubwa  katika kujenga mahusiano mazuri na yenye ufahamu mzuri. Pia ni vizuri kumuuliza mwenza wako  maswali ya kutosha . Ili tu kuwa na uhakika  kufahamu majibu yote. Ni zaidi ya mapenzi kama utajua historia ya pesa yake.

Kwa hio , kabla ya yote hakikisha unakaa na mwenza wako kuongelea masuala haya ya kipato, sio kufurahia chupa ya wine kila siku na kuondoka bila ya kujua kitu. Tambua kuwa unataka kuelekea katika safari ya pamoja, miaka 10, 20, 50, ni muda mrefu. Mazungumzo haya ni kama changamoto zingine za kuwekea msingi wa Imani yako kati yenu. huyo ndiye mtu unayempenda, hakikisha mnaongea hayo mambo yote.

Hakikisha mko katika ufalme mmoja, katika masuala ya kiroho, sio mwingine ufalme wa giza na mwingine ufalme wa Nuru.  Mzungumze kuhusu maisha , mkubaliane , na kama itaonekana kuwa hakuna makubaliano,  hakuna kulazimishana. Na mahali pa makubaliano ni katika akili zenu.

Baada ya makubaliano yote. Sasa mwili wa mke unakuwa sio mwili wake bali ni wa mwanaume, vivyo hivyo mwili wa mwanaume unakuwa wa mwanamke.

Ukweli na uadilifu , ushirikiano, kuelewana, kuwajibika, kupendana kwa dhati, bila sababu.Kuchaguana kila siku.

Suala ambalo ni la kuzuilika ni kuacha yafuatayo.

Marafiki wabaya

Uvivu

Uchungu na Hasira

Kukosa Uvumilivu.

Makubaliano yakikaa vizuri, mazungumzo  mazuri, kipato kikieleweka hakuna ndoa itakayovunjika.

Nakutakia  mafanikio katika mahusiano yako.

No comments