Kupenda Tena


Inapokuwa vigumu kupenda tena, Kumbuka kwamba moyo wako una uwezo mkubwa kuliko unavyofikiria. Unaweza kukabiliana na kitu chochote, maumivu, kuvunjwa moyo. Unajua jinsi gani ya kujiponya. Unajua jinsi gani ya kupenda japo uliumizwa  kupita kiasi.

Kumbuka kwamba moyo wako haujaharibika. Moyo wako unajifunza jinsi ya kujiponya  upya.

Wakati inapokuwa ni ngumu kupenda tena, kumbuka kwamba, Upendo ni kitu kizuri. Mara zote utakuwa ni sehemu ya historia yako  pale  unapoweka mambo sawa, unapokuwa unakufuta machozi,  pale unapokurudisha  kwenye historia ya maisha yako.Kumbuka kwamba  upendo mara zote  utakuwa ni historia  ambayo huwezi kusahau.Kumbuka historia bila ya mapenzi  huwezi kusoma.

Wakati inapokuwa ni ngumu kupenda, kumbuka  aina ya upendo ulionao kwenye maisha yako na aina ya upendo unaotoa. Fikiria kuhusu marafiki ambao hutaweza kuishi bila wao. Fikiria kuhusu wazazi wako  na jinsi gani utafanya kitu kwa ajili yao. Fikiria kuhusu watu unaowaheshimu na  kuwatamania na fikiria kuhusu  vitu ambavyo mmefanya pamoja na mtu unayempenda. kumbuka wakati ambao upendo ulikuponya, ulikufanyia wepesi katika maisha yako.

 Inapokuwa Ngumu Kupenda Tena

Wakati inapokuwa ni ngumu kupenda tena, Kumbuka  somo ulilopata la kuvunjika moyo. kumbuka jinsi ambavyo moyo ulikuteneneza kuwa mtu bora, mwenye nguvu na hekima, kumbuka wakati uliposhukuru kujijali, kusamehe, jinsi ya kutokuwa mbinafsi na  jinsi ya kuafikiana.

Wakati inapokuwa ni ngumu kupenda tena, kumbuka nyakati ambazo upendo ulikuonyesha mapenzi ya kweli. Nyakati za usiku ulizokuwa unatabasamu. Vitu vyote ulivyovifanya vya kijinga, nyimbo zote ambazo uliimba. Kumbuka kuwa  siku zako nzuri zilikuwa ni siku ambazo upendo ulikupata.

Wakati inapokuwa ni nguvu kupenda tena. Kumbuka kwamba si kila mara itakuwa ni ngumu, kwamba haitakuwa historia ya aina moja. Kumbuka kwamba  haitakuwa mchezo huo huo,  kumbuka tu kwamba ni kitu ambacho kilitokea mara ya kwanza. Njia ya pekee ya kufanya ni kupenda yalio magumu na kutunza  upendo kwa sababu hakuna  kizuri kinachotoka kwenye Uchungu na hakuna kizuri  kinachokuja  kutoka mahali ambapo hakuna utofauti.

No comments